Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Monday, July 18, 2022

IJA YAENDESHA MAFUNZO ELEKEZI KWA WATUMISHI WA MAHAKAMA

 

Mhe. Wilbard Chuma Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania leo tarehe 18/07/202 amefungua rasmi mafunzo elekezi kwa watumishi wapya 58 wa Mahakama Tanzania.  Mafunzo hayo yanaendeshwa na kufanyika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA). Hili ni kundi la kwanza kati ya waajiriwa 227 waliofanyiwa usaili na kuajiriwa na  Tume ya Utumishi wa Mahakama hivi karibuni  ambapo kuna kada mbalimbali kama Mahakimu, Maafisa Utumishi, Maafisa TEHAMA, Makatibu Mahususi, Watunza Kumbukumbu Wasaidizi  na Madereva. 

Akitoa hotuba ya ufunguzi, Mhe. Chuma alianza kwa kuwapongeza waajiriwa hao wapya kwa kuwaeleza kuwa ajira waliyopata hawakupata kama hisani ila imepatikana kutokana na ubora waliouonesha wakati wa usaili hivyo wanapaswa kuwa waaminifu, waadilifu na wachapakazi kwa kuzingatia mikataba ya ajira, viapo  na sheria za nchi katika utumishi wao.

Mhe. Chuma aliendelea kwa  kuwasisitiza Watumishi hao wapya wa Mahakama kwa kumnukuu Jaji Mkuu wa Mahakama wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma tarehe Mei 31, 2021 katika hotuba yake aliyoitoa wakati akifungua rasmi Mafunzo elekezi kwa Majaji wa Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu ya Tanzania pamoja na Mahakama Kuu Zanzibar hapa Chuoni kwa kusema watumishi wa Mahakama wanatakiwa kuwa na uadilifu na maadili ili wafanye kazi kwa kuzingaia Katiba na masharti ya viapo.

“Watu husahau kuwa mara nyingi sheria sio mbaya bali ni nafsi, maadili na tabia za wanaotekeleza sheria hizo. Hivyo nawakumbusha kila jalada utakalokuwa ukilitolea uamuzi ukumbuke kuwa linagusa watu halisi, linagusa uhuru wao, biashara zao, mali zao na familia zao. Kumbukeni kuwa wananchi kupitia katiba wametupa sisi Majaji mamlaka ya utoaji haki lakini wananchi wamebaki na haki zao zote za msingi” alinukuu.

Mhe. Chuma aliendelea kwa kuwakumbusha watumishi hao kuwa maadili ni kiini cha haki, na hivyo wakati wa kutekeleza jukumu la utoaji haki na wanatakiwa kuzingatia maadili ya kazi na kutoa maamuzi kwa kuzingatia misingi ya haki, sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo.

Mhe. Chuma aliwaeleza watumishi hao wapya  kuwa malengo ya mhimili wa Mahakama yatafikiwa iwapo watakuwa na nia moja na ushirikiano baina yao na watumishi wengine watakaowakuta kwenye vituo vya kazi watakavyopangiwa. Alieleza kwamba ushirikiano huo utasaidia kufanikisha jitihada zinazoendelea za maboresho ya Mahakama ya Tanzania. Mhe. Chuma aliwasisitiza watumishi hao kuwa na ushirikiano na wadau wengine kwa kuchukua mawazo mazuri na bora kutoka kwenye taasisi au idara zingine kwa kuyafanyia kazi au kuyafikisha mahali panapostahili ili yalete mabadiliko kwa kuwa kazi ya kulijenga taifa ni wote.

Mhe. Chuma aliendelea kwa kuwasisitiza watumishi hao kuwa dhana ya uhuru wa mahakama haina maana ya kuvunja sheria kwa kuwa kanuni hii ya kikatiba inaenda sanjari na kanuni ile ya Utawala wa Sheria. Hivyo, amewataka  Mahakimu kuwa ni wajibu wao kufanya kazi zao chini ya kivuli cha uhuru wa Mahakama, kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria za nchi na sio kwa kuzivunja. Aliendelea kwa kuwaasa watumishi wengine ambao sio  mahakimu wakawasaidie  maafisa wa Mahakama wa ngazi mbalimbali katika kufikia azma ya kutenda na kutoa haki kwa mujibu wa sheria ili wasiwe chanzo cha malalamiko au kusababisha uvunjifu wa amani kutokana na utendaji kazi  ambao unakiuka misingi ya utu na katiba.

Mafunzo  haya yanafanyika kwa makundi matatu ambapo kundi la kwanza la Mahakimu Wakazi na Maafisa Kumbukumbu Wasaidizi yamenza leo  tarehe 18 Julai ,2022.  Makundi mengine ya kada nyingine yatafuata na kutegemea kumalizika 12 Agosti, 2022.

IJA inajukumu la kuwajengea uwezo watumishi wote wa mahakama kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wao pia kwa mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yanayotoa huduma za utoaji haki  nchini.  Pamoja na mafunzo hayo Chuo kimebobea katika kutoa mafunzo ya Stashahada na Astashahada ya sheria. Vilevile Chuo kinafanya shughuli za kutoa ushauri wa kitalaamu, machapisho na tafiti mbalimbali.


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbard Chuma akifungua mafunzo elekezi kwa watumishi wapya wa Mahakama ya Tanzania yanayofanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto.





Picha za juu na chini ni watumishi wapya wa Mahakama ya Tanzania wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka wa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbard Chuma.







1.      


Thursday, July 14, 2022

TAASISI YA IRLI YAFANYA ZIARA IJA

Taasisi ya Irish Rule of Law International (IRLI) ya nchini Ireland imefanya ziara ya siku moja Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) yenye lengo la kuendeleza hatua za utekelezaji wa mkataba wa mashirikiano uliofanywa kati yake na Chuo tarehe 10 Machi, 2022.  Ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2022 ilihusisha viongozi watatu kutoka katika Taasisi hiyo ambao ni Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bwana Aonghus Kelly, Mratibu wa Programu IRLI,  Bwana Sean McHale pamoja  na  Afisa Uhusiano Mwandamizi IRLI Tanzania na Zambia, Bwana  Norville Connolly.

Wakati wa ziara hiyo wageni hawa pia walipata maelezo ya kina ya shughuli  zinazofanywa na Chuo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Chuo Bwana Goodluck Chuwa.  Bwana Chuwa alianza kwa kuwaeleza historia fupi ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto toka kilipoanzishwa na malengo ya uanzishwaji wake.  Aliendelea kwa kusema kwamba Chuo kimekuwa, msaada mkubwa sana kwa Mahakama ya Tanzania na wadau mbalimbali wa sheria nchini kwa mafunzo na tafiti mbalimbali zinazofanywa na Chuo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI nchini Tanzania Bwana  Aonghus Kelly alitoa maelezo mafupi ya Taasisi hiyo kwa kusema kuwa, Taasisi hiyo inaendesha   programu na miradi katika nchi zinazoendelea yenye lengo la kuimarisha ulinzi na upatikanaji wa haki za binadamu, demokrasia na utawala bora na kukuza utawala wa sheria. Aliendelea kwa kusema kuwa, IRLI inafanya kazi na washirika wa ndani kwa kupitia mashirikiano ili kufikia malengo yake. Alieleza kwamba washirika wa IRLI ni pamoja na mashirika ya kiserikali, wanataaluma ya sheria, watumishi wa mahakama, vyama vya wanasheria, wanafunzi wa sheria na asasi za kiraia katika nchi ambazo taasisi hiyo inafanya kazi.

Sambamba na hayo, IRLI na IJA walijadili kuhusu mpango wa kuandaa kitabu chenye mkusanyiko wa mashauri yanayohusu unyanyasaji na ukatili wa kingono kwa mtoto.

 Mkataba wa mashirikiano kati ya IRLI na IJA ni kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2022 hadi 2027 ukiwa na lengo la  kuimarisha haki ya mtoto hususani katika kufanya tafiti na mafunzo yanayolenga eneo la  unyanyasaji na ukatili wa kingono dhidi ya mtoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw. Aonghus Kelly (katikati) akiwa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa (kulia) na  Mratibu wa Programu IRLI,  Bw. Sean McHale (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Chuo walipotembelea Maktaba ya Chuo wakati wa ziara yao Chuoni.

Pichani ni wageni wa Taasisi ya IRLI na viongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto wakiwa katika Maktaba ya Chuo  wakati wa ziara.

Pichani Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa maelezo kuhusu Chuo kwa wageni kutoka IRLI wakiwa kwenye kikao cha pamoja walipofanya ziara yao Chuoni.



Picha mbalimbali za kikao kati ya wagenikutoka IRLI na Viongozi wa IJA  

 Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa zawadi ya machapisho ya Chuo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw. Aonghus Kelly.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa zawadi ya machapisho ya Chuo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw. Sean McHale .

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa zawadi ya machapisho ya Chuo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw.Norville Connolly.

Picha ya pamoja kati ya wa wageni kutoka Taasisi ya IRLI na Viongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto