Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Wednesday, December 7, 2022

JAJI MKUU AIPONGEZA IJA KWA KUANDAA VIZURI WAHITIMU WAKE

 Na: Rosena Suka IJA Lushoto

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amekipongeza Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa kuwaandaa wahitimu kwa kuwajengea ujuzi na maarifa katika fani ya sheria kwa ngazi za Stashahada na Astashahada.

 Prof. Ibrahim H. Juma ameyasema hayo kwenye mahafali ya 22 ya Chuo yaliyofanyika Chuoni hapo  leo Desemba, 7 2022. Aidha amesema kuwa wengi wa wahitimu huendelea na ngazi ya juu ya Elimu ya Sheria na huonyesha mafanikio makubwa hii inadhihirisha na  kuthibitisha ubora wa Chuo cha IJA.  Aliendelea kwa kusema  wahitimu wa Chuo wameajiriwa maeneo mbali mbali kama vile Makarani wa Mahakama; Watendaji wa Vijiji/Mitaa; Makatibu Wasaidizi katika Makampuni ya Mawakili; Wasaidizi katika Mamlaka ya Mapato Tanzania; Makatibu wa Sheria Ofisi za Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mashtaka, Serikali za Mitaa na kadhalika.

Mhe. Prof.  Juma aliendelea kuwasihi wahitimu hao kutumia  elimu waliyoipata kuibadilisha na kuisaidia jamii pale mtakapopata nafasi na uwezo wa kufanya hivyo kwani sheria inahusika na haki.

“Nawaomba mkawe watu wa haki na wenye kiu ya kutenda haki wakati wote katika yote mtakayoyafanya ili jamii ione utofauti wenu na wengine. Kutenda haki hakusubiri tu hadi uwe mtumishi wa Mahakama au mwajiriwa. Ni zoezi endelevu kwa maisha yetu”

Mhe. Prof. Ibrahim H. Juma aliendelea kuwasisitiza wahitimu hao kwa usemi wa kiingereza usemao  “Law is not always the problem. Those who implement the law may be the real problem:” na alifafanua kwa kusema kuwa sio mara zote tatizo huwa ni Sheria au kutokuwepo  kwa sheria nzuri,  bali sheria inaweza kuwa mbaya pale waliopewa dhamana ya kutekeleza sheria ili itimize malengo wanayotarajia kutoka kwa sheria husika.  Aliwaomba wahitimu wa Mahafali hayo  kuwa wasiwe na  tatizo katika utekelezaji wa sheria kwani masomo ya Stashahada ya Sheria na Astashahada ya Sheria waliyopata yamewapa mwanga wa kuelewa Sheria ili  kuweza kutumia sheria kutatua changamoto zitakazojitokeza.   

 Mhe. Prof. Ibrahim Juma aliendelea kwa kuwakumbusha wahitimu kutambua  elimu waliyonayo kuwa haitoshi kwani kasi ya maboresho na Mabadiliko ya Elimu inatakiwa ilingane na Kasi ya Mabadiliko ya Mahitaji ya Jamii.

“Watanzania wa leo wanaishi katika dunia inayosukumwa na Teknolojia yenye nguvu kubwa ya Mapinduzi ya Nne ya Viwanda (4IR). Wahitimu wenye elimu ya ngazi au daraja lolote ni lazima wahakikishe kuwa elimu waliyopata kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama haitoshi ni lazima waiboreshe kila siku ili ilingane na mahitaji ya ushindani mkubwa katika Karne ya 21”  alisema  Mhe. Prof.  Juma.

 Kwa upande mwingine, Mhe. Prof. Juma amekielekeza Chuo kwamba, katika awamu ya Pili ya Mradi wa Maboresho ya Mahakama ya Tanzania (2021-2025), kufanya maboresho ili kiwe Chuo kinachotoa elimu na mafunzo kwa wanafunzi wake na kwa watumishi wa Mahakama kwa kutumia mifumo ya  TEHAMA.  Aliendelea kwa kusema awamu ya Pili ya Maboresho ya Mahakama imetenga jumla ya Dola milioni 6 katika eneo la mafunzo ya kuongeza Ujuzi (Skills) na Maarifa (knowledge).

Aidha, Mhe. Prof. Juma amewasihi Wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo, Wahadhiri, Wakufunzi na watumishi wote wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, kujitayarisha na matumizi ya Jukwaa la Ki-elektroniki kutoa mafunzo na elimu  kwa  waliopo ndani na nje ya Chuo ambapo itaweza kutumika sio tu kwa wanafunzi wa Stashahada na Astashahada ya Sheria, bali pia litatumika kutoa mfunzo  Elekezi na Endelevu kwa Majaji, Wasajili, Naibu Wasajili, Watendaji, Mahakimu na Watumishi wa kada zote.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Gerald A. Ndika  aliwakumbusha wahitimu hao  574 kuwa kuhitimu kwao katika ngazi hizo ni mwanzo  wa safari ndefu ya kitaaluma.  Hivyo ,  na kuwaasa waendelee kutafuta elimu bila kuchoka.

 Mhe. Dkt.  Ndika alieleza kwamba kitaaluma wanachuo wa IJA wamekuwa wakifanya vizuri katika vyuo vya elimu ya juu wanapokwenda kwa ajili ya kuendelea na Masomo yao mara tu wanapohitimu IJA, Hivyo kwa ufanisi huo  inapelekea wanafunzi hao kuajiriwa katika taasisi mbalimbali za utoaji haki nchini kama vile Mahakama. 

 Naye Mkuu wa Chuo na Jaji ya Mahakama  ya Rufani, Mhe. Dkt. Paul Kihwelo ameeleza kwamba mpaka sasa Chuo kiko mstari wa mbele katika kutoa mafunzo kwa watumishi mbalimbali wa Mahakama kwa njia ya Mtandao, ambapo mafunzo haya yameweza kuwafikia watumishi wa kada ya Mahakimu na Majaji kwenye maeneo mbalimbali ya utendaji kazi.  Kwa njia ya mafunzo imeweza kupunguza gharama kwa Mahakama ya Tanzania.

Mahafali ya 22 ya IJA yameambatana na ufunguzi wa jengo la bweni la wavulana. Bweni hili  lina ghorofa nne na lina uwezo wa kulaza watu 320 na lina thamani ya shilingi za kitanzania billioni 2.6. Ujenzi wa bweni hili ulisimamiwa na Mahakama ya Tanzania katika mpango wa Maboresho ya Mahakama.


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa  hotuba wakati wa katika Mahafali ya 22 ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) leo tarehe 07 Desemba, 2022.




Wahitimu  wa Astashada ya Sheria wakiwa katika maandano ya sherehe za mahafali zilizofanyika tarehe 07 Desemba, 2022.  chuoni 

 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Ibrahim Hamis Juma na meza kuu  katika picha ya pamoja na Jumuiya ya wahitimu wa IJA (IJA ALUMN) 


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Ibrahim Hamis Juma na meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).



Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Ibrahim Hamis Juma na meza kuu  katika picha ya pamoja na baadhi  Wahitimu wa Stashahada ya Sheria kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Ibrahim Hamis Juma na meza kuu  katika picha ya pamoja na baadhi  Wahitimu wa Astashahada ya Sheria kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma  akikata utepe  kuashiria uzinduzi wa bweni la wavulana Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA). Kushoto ni  Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi  (IJA) na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Gerald Ndika,  kulia ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo.


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma  akimkabidhi mfano wa ufunguo   Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi  (IJA) na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Gerald Ndika wakati wa uzinduzi huo.

Tuesday, December 6, 2022

JUMUIYA YA WAHITIMU IJA YAENDESHA KONGAMANO LA KITAALUMA

 Na Rosena Suka, IJA

Mhe. Dkt. Gerald Ndika, Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo Desemba 6,  2022  amefungua Kongamano la Kitaaluma lililoandaliwa na Jumuiya ya Wahitimu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA ALUMNI) katika ukumbi wa Barnabas Samatta Chuoni Lushoto.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo Mhe. Dkt. Ndika alianza kwa kuwapongeza wanajumuiya hao kwa kujitolea na kushiriki katika shughuli mbalimbali zenye nia ya kutoa elimu na kukuza uelewa katika jamii kuhusiana na masuala ya sheria ikiwepo kuandaa makongomano ya kitaaluma kama hilo, kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi bure na kushiriki katika masuala mbalimbali yanayoandaliwa na Chuo kwa lengo la kuwaunganisha na kuwajengea umoja wahitimu wote wa chuo.  

Mhe. Dkt. Ndika aliendelea kwa kusema kongamano hilo ni fursa nzuri kwa washiriki kudadavua masuala muhimu yahusuyo mambo mbalimbali ya kiuchumi na ya kijamii, sambamba na kuangalia ukuaji katika maeneo ya utoaji haki.

 “ Na ni mategemeo ya Chuo na Taifa kwa ujumla kwamba kila mmoja wenu mara baada ya kuhitimu kwenu mnapaswa kuelewa kwamba nafasi nliyonayo ni vema mkaitumia katika kuleta maendeleo ya nchi na jamii kwa ujumla ili kukuza taaluma na kuielimisha jamii katika utoaji haki, mkizingatia usawa, Amani na usalama” alisema Mhe. Dkt. Ndika.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akiwa anafunga kongamano hilo aliwahimiza washiriki wa kongamano  kutumia fursa hiyo ili kuwa na mahusiano mazuri na kuitumia Jumuiya ya Wahitimu hao ili kupata fursa mbalimbali za kujifunza katika taaluma waliyonayo.

Kongamano hilo lililowashirikisha wanachuo wote lililoongozwa na mada isemayo “IJA and Prospects for offering practical legal training to lawyers Employed in Public Service ; Practicalities and Challenges” na hufanyika mara moja kila mwaka siku moja kabla ya sherehe za mahafali ya Chuo.

Mkuu wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akiwa katika picha ya pamoja na Jumuiya ya Wahitimu wa IJA  baada kufungwa kwa kongamano hilo.




Picha mbalimbali za washiriki wakiwa wanafuatilia Kongamano











Friday, November 25, 2022

IJA YATOA MAFUNZO ELEKEZI KWA SERIKALI YA WANACHUO

 Na Rosena Suka, IJA

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi Mahakama Lushoto, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo leo tarehe 25 Novemba, 2022 amefungua mafunzo elekezi ya siku moja kwa Viongozi wa Serikali ya Wanachuo wa IJA (IJASO) yaliyofanyika Chuoni Lushoto.

Katika ufunguzi huo  Mkuu wa Chuo amewaeleza viongozi hao  kwamba wanawajibu mkubwa wa kuwahudumia kwa uadilifu wanachuo wenzao  kwani wao ni kiungo  katika kufikisha yale ambayo yanatoka kwenye Uongozi wa Chuo kwenda kwa wanachuo na kutoka kwa wanachuo kwenda kwenye Uongozi wa Chuo.

Mkuu wa Chuo aliwasisitiza viongozi hao wa wanachuo kutumia vikao mbalimbali watakavyokuwa navyo ili kutatua changamoto zao na sio kulalamika au kupeleka changamoto zao kwenye mamlaka zisizohusika. Aliendelea kwa kuwataka viongozi hao kusimamia sheria, kanuni na taratibu zilizopo ili kuonyesha mfano bora kwa wanachuo wenzao,

Mkuu wa Chuo, aliwakumbusha viongozi hao kuwa na ushirikiano kati ya wao wenyewe, watumishi wa Chuo na  wanachuo wenzao bila kusahau mahusiano mazuri na jamii inayowazunguka.

Kwa upande wake Rais wa Wanachuo, Bw. Meshack D. Tupa alipokuwa akitoa shukrani zake ameushukuru Uongozi wa Chuo kwa kuandaa na kuwapatia semina hiyo elekezi na kuahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na watumishi wa Chuo na wanachuo wanaowawakilisha.

Viongozi hawa wa wanafunzi katika semina hiyo elekezi wamepitisha katika mada mbalimbali ambazo ni Masuala ya Usalama na Maadili, Unyanyasaji na Ukatili wa Kijinsia, Uongozi na Taaluma, Usimamizi wa Rasilimali za IJASO na Usitawi wa Wanachuo.

IJA imekuwa na utaratibu wa kutoa mafunzo elekezi kwa Serikali ya Wanachuo mara tu inapowekwa madarakani.


Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi Mahakama Lushoto, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akihutubia Viongozi wa Serikali ya Wanafunzi wakati wa ufunguzi wa Mafunzo Elekezi ya siku moja yaliyofanyika Chuoni Lushoto

 Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi Mahakama Lushoto, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chuo na wawezeshaji wa mafunzo elekezi. 












Pichani juu ni washiriki wa mafunzo elekezi ambao ni viongozi wa nafasi mbalimbali katika serikali ya wanachuo wakifuatilia mafunzo hayo.

Tuesday, November 8, 2022

IJA YATOA MAFUNZO YA UENDESHAJI WA MASHAURI YA MAKOSA YA KIFEDHA


Mhe. Amiri Mruma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam amefungua mafunzo ya uendeshaji wa mashauri Makosa ya Kifedha (Financial Crimes) kwa maafisa wa Mahakakama 30 katika ukumbi wa Lamada jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayo ya siku tano kuanzia leo tarehe 07/11/2022  yameandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Eastern and Southern Africa Anti-Money Laundering Group (ESAAMLG) na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).

Washiriki wa mafunzo hayo ni Majaji 14 pamoja na Mahakimu Wakazi 26 ambapo kati yao 24 ni Mahakimu Wakazi wa Mikoa Tanzania Bara. Lengo la mafunzo hayo ni kuwafanya washiriki hao waweze kubadilishana uzoefu kwenye maeneo mbalimbali ya sheria za kimataifa na kitaifa za biashara haramu ya wanyamapori, ufadhili wa ugaidi na utakatishaji fedha, kuangalia madhara ya makossa hayo katika taifa na dunia,   urejeshaji wa mali zilizopatikana kutokana na makosa hayo, wajibu wa Maafisa wa Mahakama, wapelelezi na waendesha mashtaka katika uendeshaji wa mashauri yahusuyo makosa hayo n.k.

Wawezeshaji wa mafunzo hayo ni baadhi ya majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, ofisi ya Mashtaka ya Taifa, Wizara ya Maliasili na Utalii, PPRA, wawezeshaji kutoka mamlaka za wanyamapori za baadhi ya nchi barani Afrika na wawezeshaji wabobevu kutoka mataifa mbalimbali duniani.

Mafunzo haya ni muendelezo wa mafunzo mengine kama hayo yaliyotolewa kwa kundi la kwanza la Mahakimu 40 mwezi Septemba mwaka  huu.

Pichani juu Mhe. Amiri Mruma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam (katikati) alipokuwa anafungua mafunzo ya mafunzo ya uendeshaji wa mashauri Makosa ya Kifedha (Financial Crimes) kwa maafisa wa Mahakama kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara ambao wanaonekana kwenye picha za chini.








Monday, October 24, 2022

IJA YAENDESHA MAFUNZO YA NAMNA BORA YA UENDESHAJI WA MASHAURI YA WANYAMAPORI NA MISITU

Na; Rosena Suka  IJA Lushoto

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tanga, Latifa Mansour leo 24 Oktoba, 2022 amefungua mafunzo ya uendeshaji wa mashauri ya makosa dhidi ya wanyamapori ikiwepo ujangiri na makosa yanayohusiana na hayo kwa wadau wa haki jinai. Mafunzo hayo yanaendeshwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania kwa ufadhili wa PAMS Foundation.   

Mafunzo hayo ya siku tano ni mtiririko wa mafunzo mengine kama hayo yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 10 hadi 14 Oktoba 2022 kwa kundi la kwanza lililojumuisha Majaji wa Mahakama Kuu, Waendesha Mashtaka Waandamizi na Wapelelezi Waandamizi, na kufuatiwa na kundi la pili  la mahakimu, waendesha mashtaka na wapelelezi kuanzia tarehe 17 hadi 21 Oktoba 2022. Hili ni kundi la tatu na mwisho ambalo linashiriki mafunzo hayo katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto ambayo yanahitimishwa.

Akiongea wakati wa ufunguzi Mhe. Latifa Mansour alieleza kuwa mafunzo haya yana lengo la kuwaleta pamoja wadau wa utoaji haki jinai na kubadilishana uzoefu kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo sheria za kimataifa na kitaifa za wanyamapori na misitu ikiwemo  upelelezi na uendeshaji wa mashauri ya makosa dhidi ya wanyamapori na makosa yanayohusiana na hayo.

Aidha, Mhe. Mansour aliongeza kwa kusema kuwa mafunzo haya yatawawezesha wapelelezi namna ya kufanya upelelezi kama sheria inavyotaka ili kuwezesha kesi za namna hiyo zinapofikishwa Mahakamani na waendesha mashitaka ziwe na ushahidi wa kutosha na kutokutoa mwanya kwa mtu aliyefanya kosa kukwepa kwa visingizio mbalimbali.

 “Tunaamini kwamba kama Mahakama pamoja na upelelezi itashirikiana na kuhakikisha kwamba hawa watakaobainika na makosa hayo watachukuliwa hatua zipasazo na wanapata adhabu za kutosha ili iwe funzo kwa jamii yote na wale wote wanaofanya biashara hizi haramu.” Alisema Jaji huyo.

Naye mwakilishi wa PAMS Foundation, Bw. Samson Kassala alieleza kuwa  Taasisi hiyo isiyo ya kiserikali inajishughulisha na masuala ya uhifadhi wa mazingira na usalama wa wanyamapori.   Makao  Makuu ya Taasisi hiyo yako jijini Arusha. Bw. Kassala alifafanua kwa kusema PAMS Foundation imekuwa ikisaidia katika kuwajengea uwezo wale wote walio mstari wa mbele katika kulinda  ulinzi wa maliasili zetu kwa manufaa ya wananchi na vizazi vijavyo kama sheria za nchi zinavyosema.

Bw. Kassala aliendelea kwa kusema kuwa PAMS Foundation imeendelea  kushirikiana na Serikali na wanafanya hivyo ili kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania kwenye maeneo mengi ikiwemo utalii na hasa baada ya ziara ya Utalii (Royal Tour) ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano kati ya IJA na PAMS Foundation ambayo yalisainiwa tarehe 23/06/2022 jijini Dar es Salaam kati ya Mkuu wa Chuo pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa PAMS Foundation.



Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga, Latifa Mansour akiwa anafungua mafunzo ya uendeshaji wa mashauri ya makosa dhidi ya wanyamapori yanayofanyika  Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA)



Picha mbalimbali za washiriki wa mafunzo ya uendeshaji wa mashauri ya makosa dhidi ya wanyamapori yanayofanyika  Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) wakiwafuatilia hotuba ya Mgeni rasmi wakati wa ufunguzi.





Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga, Latifa Mansour akiwa katika picha pamoja ya washiriki wa mafunzo ya uendeshaji wa mashauri ya makosa dhidi ya wanyamapori yanayofanyika  Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).  Waliokaa kutoka kulia ni Bw. Goodluck Chuwa, Makamu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, kulia zaidi ni Mhe. Awadhi Mohamed, Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Na kutoka kushoto ni Bw. Samsoni Kassala, Mkurugenzi wa Mafunzo na Tafiti PAMS Foundation (Mafunzo), kushoto zaidi ni Bw. Elisifia  Ngowi, Mkurugenzi wa Intelijensia na Oparationi  PAMS Foundation.

Wednesday, October 19, 2022

WAJUMBE WA BARAZA LA UONGOZI W CHUO WATEMBELEA BWENI LA WAVULANA IJA

Habari Picha


Muonekano wa mbele wa bweni la wavulana lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 360 

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dr.  Gerald Ndika (Mwenye Tai Nyekundu) akiwa pamoja na wajumbe wa Baraza la Uongozi na wajumbe wa menejimenti ya Ija walipotembela Bweni la wavulana hivi karibuni IJA


Wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Wajumbe wa Menejimenti wakiwa kwenye ziara hiyo




         Wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Wajumbe wa Menejimenti wakipita kwenye maeneo                                             mbalimbali ya jengo hilo wakati wa ziara 

 Wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Wajumbe wa Menejimenti wakipita kwenye maeneo                                             mbalimbali ya jengo hilo wakati wa ziara 

 Wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Wajumbe wa Menejimenti wakipita kwenye maeneo                                             mbalimbali ya jengo hilo wakati wa ziara 
 Wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Wajumbe wa Menejimenti wakipita kwenye maeneo                                             mbalimbali ya jengo hilo wakati wa ziara 
 

Wednesday, August 31, 2022

JAJI MKUU WA TANZANIA ASISITIZA MAADILI KWA MAJAJI

 Na Rosena Suka IJA

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma jana tarehe 30 Agosti, 2022 alifungua mafunzo elekezi yanayowaleta pamoja Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wapya 21 na wengine wanne wa Mahakama Kuu Zanzibar ambapo amewahimiza kuzingatia maadili wanapotekeleza majukumu yao ya utoaji haki kwa wananchi.

Mhe. Prof. Juma aliwataka Majaji hao kusoma na kujadili miongoni mwao Kanuni za Maadili za Maafisa Mahakama iliyochapishwa tarehe 20 Novemba, 2020 kupitia Tangazo la Serikali Namba 1001 la mwaka 2020 ambazo zitawasaidia kubaki ndani ya matarajio ya kimaadili.

“Uwezo na Maadili ni nguzomuhimu ya kuaminiwa na kuaminika kwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Uwezo, Ujuzi na Maarifa yenu yatajenga Imani na kuaminiwa kwenu kwa namna ambavyo mtafanya maamuzi yenu kwa haki, kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, Taratibu, Miongozo, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema.

Jaji Mkuu akawakumbusha kuwa pamoja na maadili ya Viongozi wa Umma; Majaji wa Mahakama Kuu, Majaji wa Rufani, Wasajili, Mahakimu, na Wasaidizi wote wa Majaji, wanaongozwa na Kanuni za Maadili za Maafisa wa Mahakama (Code of Conduct and Ethics for Judicial Officers, 2020).

Amesema uongozi wa Mahakama ukishirikiana na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), umeweka utaratibu wa Mafunzo elekezi ya awali kwa wote walioapishwa kuwa Majaji wakiwemo wale wanaojiunga na utumishi wa Mahakama kwa mara ya kwanza.

“Mafunzo elekezi yanalenga kuwatayarisha kutumikia nafasi ya Jaji. Mafunzo elekezi yanawakaribisha rasmi katika Utumishi wa Mahakama wenye maudhui, tamaduni, mitizamo na uzoefu uliojengeka muda mrefu ambazo itawawekea misingi imara ya kuwasaidia katika utoaji wa huduma za kimahakama,” amesema.

Jaji Mkuu amebainisha pia kuwa mafunzo hayo elekezi yanalenga kuwajengea msingi wa kuifahamu Mahakama, kufahamu mwelekeo wa Mhimili wa Mahakama ndani ya maudhui ya mwelekeo wa nchi ya Tanzania ndani dunia inayoizunguka.

Akaseama kuwa kwa upande wake Mhimili wa Mahakama utafaidika na uwezo, uzoefu, ujuzi na umahiri wa Majaji hao waliojijengea kutoka maeneo waliyopitia, hivyo mchanganyiko huo utakuwa wa faida kubwa kwao binafsi, kwa Mahakama na pia kwa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Jambo moja muhimu ambalo litajitokeza katika Mafunzo haya elekezi ni dhamira dhahiri ya Mahakama ya Tanzania kuwaingiza kuwa sehemu ya waboreshaji wa huduma za utoaji haki kupitia Mipango Mkakati na Programu za Maboresho,” Mhe. Prof. Juma alisema.

Amesema kuwa Maboresho ya Mahakama yanayoendelea hivi sasa yamewajengea watumishi wa Mahakama utamaduni mpya, mitazamo mipya na mwelekeo mpya wa utoaji wa huduma za haki kwa kumlenga na kumridhisha mwananchi (Citizen-Centric Judicial Modernization and Justice Service Delivery).

“Ninawasihi muwe sehemu ya dhana hii ya utoaji wa huduma za haki kwa kumlenga na kumridhisha mwananchi. Mafunzo haya elekezi yanawatayarisha Majaji wapya kuifahamu Dira ya Mahakama ya Tanzania—Timely and Accessible Justice for All,” Jaji Mkuu alisema.

Aidha, Mhe. Prof. Juma akabainisha kuwa katika kumlenga na kumridhisha mwananchi, Jaji sio idadi bali umuhimu wake kwa mwananchi ni huduma bora za haki, ujuzi, ufanisi, na uwazi wa huduma za utoaji haki kwani wananchi wanafuata huduma mahakamani, wala hawaji kumtembelea Jaji, wanafuata huduma za utoaji haki.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma  akifungua Mafunzo Elekezi kwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu Zanzibar uliofanyika tarehe 30 Agosti, 2022 katika Ukumbi wa mikutano wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma. Kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto,(IJA)  Mhe. Dkt. Gerald Ndika na kulia ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe Mustapher Siyani






Picha ya chini na ya juu ni Sehemu ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Zanzibar wakimsikiliza Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (hayupo pichani)


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Zanzibar mara baada ya kufungua mafunzo elekezi. Wengine walioketi mbele ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe Mustapher Siyani (wa tatu kulia),Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) Lushoto, Mhe. Dkt. Gerald Ndika (wa tatu kushoto), Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) Lushoto, Mhe. Dkt. Faustine Kihwelo (wa pili kushoto), Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (wa pili kulia), Mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi (wa kwanza kushoto) na Mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Wakili Genoveva Katto.



Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji Wanawake wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Zanzibar mara baada ya kufungua mafunzo elekezi kwa Majaji.