Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Wednesday, May 17, 2023

WANANCHI WAIMWAGIA SIFA IJA KWA ELIMU BORA YA SHERIA

 Na: Yusuph  Sungura  IJA  Lushoto

Wananchi mbalimbali wamekipongeza Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) kwa utoaji wa elimu bora ya sheria hapa nchini. Wananchi hao wametoa pongezi hizo walipotembelea banda la IJA katika maonesho ya pili ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi(NACTVET) ya mwaka 2023, yanayoendelea katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Erick Samwel ambae ni mkazi wa Arusha amesema kuwa IJA inatoa elimu bora ya sheria nchini na kwamba kinastahili pongezi kwa kazi hiyo.

"Kuna ndugu yangu alisoma hapo IJA miaka ya nyuma, anasema kuwa chuo hicho kinafundisha sana na kumfanya mwanafunzi awe vizuri sana kwenye sheria," amesema Samwel.

Nae mzazi Martha Shirima aliyefika kwenye banda la chuo cha IJA na binti yake, amesema kuwa wamefika ili kuulizia utaratibu wa kujiunga na chuo hicho kwa kuwa anasikia walimu wanafundisha sana kiasi ambacho mwanafunzi anakuwa mahiri sana.

"Nimekuwa nikisikia kutoka kwa baadhi ya watu wakikisifu sana hiki chuo kwa elimu ya sheria nchini, ndio maana nimekuja hapa na binti yangu ili tupate maelezo zaidi. Hongereni kwa hilo," amesema Martha.

Kwa upande wake Mhadhiri Msaidizi wa IJA Tundonde Mwihomeke amebainisha kuwa IJA ni bora katika utoaji wa elimu ya sheria nchini kwa kuwa walimu wake wamekuwa wakihakikisha mwanafunzi anaelewa zaidi.

"Walimu wa IJa tunahakikisha wanafunzi anaelewa, watu wanasema hatuna blah blah, ni kweli, lengo letu ni kuhakikisha mwanafunzi anapata elimu bora iendane na dunia inavyokwenda," amesimulia mhadhiri huyo msaidizi Tundonde.

Pia ameongeza kuwa kila mwanachuo hupangiwa mhadhiri anaewajibika kumuongoza na kumshauri katika masuala ya taalumu yake.

Nae Afisa Udahili wa chuo cha IJA, Magdalena Mlumbe amesema kuwa chuo kina miundombinu muhimu na ya kisasa ikiwemo maktaba ambayo ina vitabu muhimu katika maarifa ya sheria.

"Chuo chetu kina miundombinu ya kisasa ambayo ni muhimu katika ufundishaji, mathalani kuna maktaba ya kisasa yenye vitabu vya ambavyo si rahisi kuvipata kwenye maktaba zingine," amesema Magdalena.

Vile vile, Magdalena ameongeza kuwa chuo kina miundombinu yote muhimu ikiwemo huduma ya malazi, zanahati na viwanja vya michezo.


Pichani Bi Tundonde Mwihomeke Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto akitoa maelezo ya shughuli za Chuo kwa wananchi waliojitokeza katika banda la Chuo wakati wa Maonesho ya Pili ya ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi(NACTVET) ya mwaka 2023.

Pichani Bi Magdalena Mlumbe Afisa Udahili wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto akitoa maelezo ya shughuli za Chuo kwa wananchi waliojitokeza katika banda la Chuo wakati wa Maonesho ya Pili ya ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi(NACTVET) ya mwaka 2023.


Pichani Bi Tundonde Mwihomeke Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto akitoa maelezo ya shughuli za Chuo kwa wanafunzi waliojitokeza katika banda la Chuo wakati wa Maonesho ya Pili ya ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi(NACTVET) ya mwaka 2023.



Pichani wanafunzi waliotembelea banda la Chuo wakipata maelezo kuhusu shughuli za Chuo wakati wa Maonesho ya Pili ya ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi(NACTVET) ya mwaka 2023.

Thursday, May 4, 2023

WANACHUO IJA WAFANYA ZIARA BUNGENI

Wanachuo 50 wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) leo  Mei, 4 2023 wamefanyia ziara ya kimasomo ya  siku moja  katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma.

Sambamba na ziara hiyo  wanachuo hawa wamepata fursa ya kutembelea Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki  cha Morogoro walipokuwa safarini kuelekea Dodoma ambapo kwenye kituo hicho walipata fursa ya kuona shughuli mbalimbali za kimahakama zinavyoendeshwa.

Wakiongea  baada ya ziara yao Bungeni  wanachuo hao wa IJA wameupongeza Uongozi wa Chuo, watumishi wa kituo Jumuishi cha Mahakama Morogoro kwa kufanikisha ziara hiyo.

Pia wametoa shukrani nyingi kwa Mbunge wa Lushoto Mhe. Shaban Shekilindi Kwa kuwa mwenyeji wao walipotembelea bungeni kwa kusema kwamba wamepata mafanikio makubwa na wamejifunza mambo mengi kuhusu mwenendo wa Bunge pamoja ma historia ya bunge hilo.

Wanachuo hao wakiwa wameambatana na walezi wao wa Chuo Bi. Frida  Nicholaus na Bw. George  Banoba kesho  tarehe Mei, 5 2023  watapata nafasi nyingine ya kutembelea  Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki cha  Dodoma.



Pichani ya juu na chini ni Wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) wakiwa ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia mjadala Bungeni walipofanya ziara Bungeni Jijini Dodoma.




Wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) wakitoka  nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya kuhudhuria kikao cha Bunge walipofanya ziara Bungeni Jijini Dodoma.

Picha mbalimbali za Wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge walipofanya ziara Bungeni Jijini Dodoma.


Picha mbalimbali za Wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge walipofanya ziara Bungeni Jijini Dodoma.



 


 Wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi walipofanya ziara Bungeni Jijini Dodoma.





 

Tuesday, May 2, 2023

IJA YAADHIMISHA MEIMOSI KWA KUMUAGA MTUMISHI ANAYESTAAFU

Na; Yusuphu Sungura IJA

Chuo cha Uongozi wa Mahakama  Lushoto(IJA) leo Mei, 1 2023 kimeungana na wafanyakazi duniani kote katika kuadhimisha siku ya wafanyakazi. Sherehe hizi zilizoandaliwa na Uongozi wa Chuo zilifanyika katika ukumbi wa Ibrahim Hamis Juma uliopo chuoni Lushoto.

 Watumishi wa IJA pamoja na watumishi kutoka Mahakama ya Wilaya ya Lushoto  waliungana pamoja katika kuadhimisha sherehe hii iliyoambatana na matukio mbalimbali ambayo ni kumwaga rasmi mtumishi wa muda mrefu Dokta Joseph Ismail Hokororo ambae amestaafu kwa hiara.  Pamoja na shughuli hiyo pia sherehe hii ilijumuisha kuwakaribisha watumishi wageni waliohamia na watumishi wapya katika utumishi wa umma.

 Akitoa neno katika sherehe hizo kwa niaba ya mkuu wa chuo,  makamu mkuu wa Chuo, taaluma, utafiti na ushauri, Bwana Goodluck Chuwa amewanasihi wafanyakazi wote kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na umoja. Aidha amewataka watumishi wapya waliyojiunga na IJA kufuata miongozo na kanuni za utumishi wa umma, pamoja na kufanya kazi kwa bidii ili kuleta tija kwa maendeleo ya chuo.

 Akielezea Kuhusu mtumishi anaegwa, Bwn. Chuwa amemsifu kuwa alikuwa mtumishi mwema, mvumilivu na aliyeipenda kazi yake kwa dhati. Vile vile, amesema kuwa Dokta Hokororo ni mtumishi aliyesaidia kuikuza lugha ya kiswahili IJA kwa kushajiisha  maneno kama udahili, mchakato na mdau.

Nae mtumishi aliyeagwa, Dkt. Hokororo amewashukuru watumishi wote wa IJA kwa ushirikiano wao mkubwa waliyompa katika kipindi chake chote cha utumishi chuoni hapa cha takribani miaka 20. Pia amemshukuru Mkuu wa Chuo, Mhe. Dkt.  Paul F. Kihwelo ambae ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, kwa ushauri na ushirikiano aliyempatia kwa kipindi chake chote cha kufanya kazi IJA.

 "Binafsi amekuwa msaada mkubwa kwangu hasa nilipopata changamoto za kibinafsi, nimekuwa nikienda ofisini kwake kumshirikisha jambo lililonitatiza, nae bila kusita alinipa msaada mkubwa na wakati wote alinisisitiza kumtegemea Mungu kwa kila jambo," amesimulia Dkt. Hokororo.

 Shughuli hiyo imeambatana pia na tukio la kumtangaza na kumpa zawadi mfanyakazi bora wa IJA mwaka 2022/2023, ambae ni bwana Wilson Msoffe wa idara ya uhasibu.  Bwana Msoffe ametunukiwa fedha tasilimu shilingi milioni moja, Cheti na picha yake kubwa itakaa kwenye mbao ya matangazo kwa muda wa mwaka mmoja ili kutambulika kama mfanyakazi bora wa mwaka 2023. Sambamba na hilo,  chuo kimewapa zawadi wafanyakazi hodari wanne (4)  ambao ni George Masanja(Afisa Milki), Mustafa Maghembe(Dereva), Dorothea Kavuye(Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Maktaba) na Cheusi Waziri(Katibu Mukhtasi). Kila mmoja amezawadiwa fedha taslimu  shilingi laki tatu.

Picha mbalimbali za Sherehe za Mei Mosi