Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Thursday, July 14, 2022

TAASISI YA IRLI YAFANYA ZIARA IJA

Taasisi ya Irish Rule of Law International (IRLI) ya nchini Ireland imefanya ziara ya siku moja Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) yenye lengo la kuendeleza hatua za utekelezaji wa mkataba wa mashirikiano uliofanywa kati yake na Chuo tarehe 10 Machi, 2022.  Ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2022 ilihusisha viongozi watatu kutoka katika Taasisi hiyo ambao ni Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bwana Aonghus Kelly, Mratibu wa Programu IRLI,  Bwana Sean McHale pamoja  na  Afisa Uhusiano Mwandamizi IRLI Tanzania na Zambia, Bwana  Norville Connolly.

Wakati wa ziara hiyo wageni hawa pia walipata maelezo ya kina ya shughuli  zinazofanywa na Chuo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Chuo Bwana Goodluck Chuwa.  Bwana Chuwa alianza kwa kuwaeleza historia fupi ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto toka kilipoanzishwa na malengo ya uanzishwaji wake.  Aliendelea kwa kusema kwamba Chuo kimekuwa, msaada mkubwa sana kwa Mahakama ya Tanzania na wadau mbalimbali wa sheria nchini kwa mafunzo na tafiti mbalimbali zinazofanywa na Chuo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI nchini Tanzania Bwana  Aonghus Kelly alitoa maelezo mafupi ya Taasisi hiyo kwa kusema kuwa, Taasisi hiyo inaendesha   programu na miradi katika nchi zinazoendelea yenye lengo la kuimarisha ulinzi na upatikanaji wa haki za binadamu, demokrasia na utawala bora na kukuza utawala wa sheria. Aliendelea kwa kusema kuwa, IRLI inafanya kazi na washirika wa ndani kwa kupitia mashirikiano ili kufikia malengo yake. Alieleza kwamba washirika wa IRLI ni pamoja na mashirika ya kiserikali, wanataaluma ya sheria, watumishi wa mahakama, vyama vya wanasheria, wanafunzi wa sheria na asasi za kiraia katika nchi ambazo taasisi hiyo inafanya kazi.

Sambamba na hayo, IRLI na IJA walijadili kuhusu mpango wa kuandaa kitabu chenye mkusanyiko wa mashauri yanayohusu unyanyasaji na ukatili wa kingono kwa mtoto.

 Mkataba wa mashirikiano kati ya IRLI na IJA ni kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2022 hadi 2027 ukiwa na lengo la  kuimarisha haki ya mtoto hususani katika kufanya tafiti na mafunzo yanayolenga eneo la  unyanyasaji na ukatili wa kingono dhidi ya mtoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw. Aonghus Kelly (katikati) akiwa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa (kulia) na  Mratibu wa Programu IRLI,  Bw. Sean McHale (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Chuo walipotembelea Maktaba ya Chuo wakati wa ziara yao Chuoni.

Pichani ni wageni wa Taasisi ya IRLI na viongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto wakiwa katika Maktaba ya Chuo  wakati wa ziara.

Pichani Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa maelezo kuhusu Chuo kwa wageni kutoka IRLI wakiwa kwenye kikao cha pamoja walipofanya ziara yao Chuoni.



Picha mbalimbali za kikao kati ya wagenikutoka IRLI na Viongozi wa IJA  

 Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa zawadi ya machapisho ya Chuo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw. Aonghus Kelly.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa zawadi ya machapisho ya Chuo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw. Sean McHale .

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Bw. Goodluck Chuwa akitoa zawadi ya machapisho ya Chuo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IRLI Bw.Norville Connolly.

Picha ya pamoja kati ya wa wageni kutoka Taasisi ya IRLI na Viongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto 

0 comments:

Post a Comment