Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Monday, March 6, 2023

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AFANYA ZIARA IJA

 

Leo tarehe 6 Machi, 2023 Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, Waziri wa Katiba na Sheria amefanya ziara ya siku moja katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa kutembelea maeneo mbalimbali na kuona shughuli zinazofanyika chuoni na alipata wasaa wa kuongea na Menejimenti ya Chuo na Watumishi katika ukumbi wa mafunzo wa Ibrahim Hamis Juma.   Katika ziara hjyo Mhe. Dkt. Ndumbaro ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Khatibu Kazungu

Akizungumza na Menejimenti na Watumishi Mhe. Dkt. Ndumbaro ametoa salamu za pongezi kwa Chuo kwa kufanya majukumu yake ya msingi kama sheria ya uanzishwaji wake ilivyotaka.  Kwani kwa sasa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto ndicho Chuo pekee kilichobaki kwenye misingi yake hapa Tanzania.

Aliendelea kwa kusema kwamba, uimara na ubora wa Mhimili wa Mahakama umetokana na ubora Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa kutoa mafunzo ya kujengea uwezo watumishi wa Kada mbalimbali wa Mhimili wa Mahakama na wadau wengine wa Sheria nchini, hivyo amekitaka Chuo kupanua wigo nje ya mipaka ya Tanzania ili kujipatia sifa chenyewe, Mhimili wa Mahakama na Tanzania kwa ujumla.

Mhe. Dkt. Ndumbaro aliendelea kwa kutoa wito kwa watumishi kufanya kazi kwa bidii na kuheshimu haki na misingi ya mtumishi wa umma katika utendaji wa kazi zao za kila siku. Mhe. Dkt. Ndumbaro alisema “Utumishi wa Umma unaongozwa na Katiba, Miongozo  na mila na desturi” alisema Mhe. Dkt. Ndumbao.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Dkt. Gerald A. Ndika katika salamu zake amemshukuru Mhe. Dkt. Ndumbaro na Dkt. Kazungu kwa kufanya ziara hiyo ya kutembelea Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto.  Mhe. Dkt. Ndika aliendelea kwa kusema kwamba matarajio ya Mhimili wa Mahakama kwa Chuo yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa Chuo kuwa kitovu cha mafunzo ya watumishi wa mahakama na Chuo kimekuwa kikitoa machapisho mbalimbali yanayosaidia katika utendaji kazi wa kila siku wa watumishi wa mahakama hususani Majaji na Mahakimu.  

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo alisema Chuo kwa sasa kinaendesha mafunzo mbalimbali ya kuwajengea uwezo watumishi wa mahakama ili kuendana kasi ya Mhimili wa Mahakama. Na aliendelea kwa kusema Chuo kimefanya mafunzo mengi ya aina mbalimbali kwa njia ya mtandao, kwakufanya mafunzo kwa njia imekuwa ikitoa mafunzo idadi kubwa ya watumishi wa  mahakama  na kwa wakati hivyo kupelekea Mahakama  kupunguza mzigo mkubwa bajeti ya mafunzo kwa watumishi.

Mhe. Dkt. Kihwelo aliendelea kwa kusema Chuo kimekuwa kikifanya vizuri katika utoaji wa mafunzo toka kilipoanzishwa na kupelekea wahitimu wengi kupata teuzi mbalimbali na kuajiriwa katika taasisi mbalimbali za utoaji haki na Mhimili wa Mahakama.

 

Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, Waziri wa Katiba na Sheria akihutubia Watumishi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto alipofanya ziara ya Chuoni
 


Mkuu wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akitoa historia fupi ya Chuo 


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Khatibu Kazungu akitoa salamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria alipokuwa ameambatana na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro.

Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, Waziri wa Katiba na Sheria akipanda mti kwenye bustani ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto alipofanya ziara ya Chuoni.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Dkt. Gerald A. Ndika akimkabidhi zawadi ya machapisho yanayozalishwa na Chuo Naibu Katibu Mkuu  Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu.

Pichani ni baadhi ya Watumishi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro alipofanya ziara chuoni.


Picha ya pamoja ya meza kuu na wajumbe wa Menejimenti ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto

Picha ya pamoja ya meza kuu na wajumbe wa Halmashauri ya RAAWU Tawi la IJA


Picha ya pamoja ya meza kuu na watumishi waliofanya kazi Chuoni toka Chuo kilipoanzishwa


Picha ya juu na chini meza kuu  na watumishi waliohudhuria kikao wakati wa ziara ya Waziri