Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Monday, August 14, 2023

Msajili mkuu wa Mahakama ya Tanzania afungua Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu Wakazi wapya 37

 

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma amefungua Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu wakazi wapya 37 wa Mahakama za Mwanzo leo tarehe 14/08/2023.

Mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Mahakama ya Tanzania na kuendeshwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) yanafanyika hapa Chuoni IJA na yatadumu kwa siku tano hadi tarehe 18/08/2023.

Katika hotuba yake ya Ufunguzi Mhe. Chuma ambae ndiye alikuwa mgeni Rasmi  amewataka Mahakimu hao kwenda kusaidia kuondoa mrundikano wa mashauri katika Mahakama za mwanzo kama ambavyo Sera ya Mahakama ya Tanzania inavyotaka.

“Mpaka sasa bado Mahakama za Mwanzo zinaendelea kuongoza katika umalizaji wa Mashauri na kutokuwa na mrundikano wa mashauri, kwa hiyo tunategemea ongezeko lenu litaendelea kupunguza mzigo wa kazi wa kila hakimu na hatimaye kuendeleza sera ya Mahakama ya Tanzania kutaka kusiwe na mashauri yanayozidi miezi sita,” amesema Mhe. Chuma.

Pia Mhe. Chuma amewataka mahakimu wakazi hao wapya kujifunza matumizi ya Teknolojia ya habari na Mawasiliano(TEHAMA) ili waweze kutekeleza vema majukumu yao hasa wakati huu Mahakama ya Tanzania ikiwa imejielekeza katika eneo hilo la Teknolojia.

“Karne hii ya 21 imetawaliwa na matumizi ya Teknolojia katika kuwahudumia wananchi, jifunzeni matumizi ya mifumo ya TEHAMA inayoendeshwa na Mahakama ili msipate ugumu mnapotekeleza majukumu yenu,” amesisitiza Mhe. Chuma.

Vile vile, Mhe. Chuma amewasisitiza washirika hao kuwa wanapotekeleza majukumu yao, basi hawana budi kuzingatia misingi ya haki za binadamu, maisha ya watu na ustawi wa Usalama wa nchi.

Kwa upande wake Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama IJA, Mhe. Dkt. Patricia Kisinda amezungumzia muhimu wa mafunzo hayo kwa kubainisha kwamba yanalenga kuwapatia Mahakimu hao miongozo itakayowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Kimsingi umuhimu wa mafunzo haya ni kwa ajili ya kuwapatia muongozo Mahakimu wapya ambao wanaenda kuanza majukumu yao katika Mahakama za mwanzo, ukiwemo utoaji wa haki ambao ndio jukumu kubwa la Mahakimu hawa,” amesema Mhe. Dkt. Kisinda.

Ameongeza kuwa Mahakimu watapewa miongozo, maelekezo na miiko mbalimbali ambayo inahusiana na majukumu ya kule wanapokwenda kusimamia utoaji wa haki.

Nao baadhi ya Washiriki wa Mafunzo hayo akiwemo  Mhe. Aden William Ruvurahende ambae ni Hakimu Mkazi mpya amebainisha faida ya mafunzo hayo kwao wao washiriki.

“Kwa kweli suala hili la mafunzo kwetu sisi ni la muhimu sana kwa sababu ni mwanzo wa kujua majukumu yetu, na fursa ya kufahamu miongozo na kanuni  ya kimahakama  ili itusaidie kwa ajili ya utendaji haki pale tunapokwenda kuwahudumia wananchi,” amesema Mhe. Ruvurahende.

 Kuhusiana na mlundikano wa mashauri amebaininisha: “Kuhusiana na mrundikano wa mashauri Mahakamani, ni changamoto kwetu sisi ila tunakwenda kusaidia kutatua suala hilo.”

Nae Mshiriki Mhe. Salma Athuman Mwamende anabainisha kuwa Mahakama itarajie weledi, ufanisi, na uwajibikaji kutoka kwao.

 



Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma akihutubia wakati wa Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu wakazi wapya 37 wa Mahakama za Mwanzo yanayofanyika Chuoni IJA Lushoto.


Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama katika Chuo cha IJA, Mhe. Dkt. Patricia Kisinda akizungumza wakati wa Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu Wakazi wapya wa Mahakama za Mwanzo yanayofanyika Chuoni IJA Lushoto.



Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma(katikati) wakati wa Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu wakazi wapya 37 wa Mahakama za Mwanzo yanayofanyika Chuoni IJA Lushoto.

Wa pili kushoto ni  Mhe. Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama katika Chuo cha IJA, Mhe. Dkt. Patricia Kisinda, wa Pili kulia ni Mkurugenzi wa Msaidizi wa Mafunzo ya Mahakama ya Tanzania, Mhe. Bi. Patricia Ngungulu, wa kwanza kulia ni  Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto Mhe. Rose Ngoka na wa kwanza kushoto ni Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto Mhe. Kavumo Mndeme.




Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma(katikati) akiwa katika picha na baadhi ya baadhi ya Washiriki wa Mafunzo Elekezi ambao ni Wahe. Mahakimu Wakazi wapya wa mahakama za Mwanzo katika Chuo Cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA).

Wa pili kushoto ni  Mhe. Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama katika Chuo cha IJA, Mhe. Dkt. Patricia Kisinda, wa Pili kulia ni Mkurugenzi wa Msaidizi wa Mafunzo ya Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu, wa kwanza kulia ni  Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto Mhe. Rose Ngoka na wa kwanza kushoto ni Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto Mhe. Kavumo Mndeme.




Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo Elekezi ambao ni Wahe. Mahakimu Wakazi wapya wa mahakama za Mwanzo wakiwa katika mafunzo hayo katika Chuo Cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA).





Jaji mstaafu ambae pia ni Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheira, Mhe. January Msoffe akiwasilisha mada kwa Washiriki wa Mafunzo Elekezi ambao ni Mahakimu Wakazi wapya wa Mahakama za Mwanzo yanayofanyika katika Chuo Cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA).


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma akihutubia wakati wa Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu wakazi wapya 37 wa Mahakama za Mwanzo yanayofanyika Chuoni IJA Lushoto.


Sunday, August 6, 2023

Naibu Waziri: IJA ni Chuo muhimu kwenye mambo ya haki






Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul amesema kuwa Chuo cha Uongozi wa MahakamaLushoto(IJA) ni Chuo muhimu katika kuwajenga watu wanaosimamia masuala ya haki hapa nchini.
Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul amesema hayo leo Jumamosi tarehe 05/08/2023 wakati akizungumza na wajumbe wa Menejimenti ya IJA,  Halmashauri Tendaji ya Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti(RAAWU) tawi la Lushoto pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, hapa Chuoni wilayani Lushoto.
Amesema kuwa Chuo cha IJA kinapotoa maarifa kwa watu wa kada mbalimbali, basi kinasaidia katika masuala ya haki, akibainisha kuwa wananchi mbalimbali bado wanakabiliwa na ukosefu wa haki.
"IJA ni Chuo muhimu, nimefurahi kuona kumbe tuna Taasisi nzuri hapa," amesema Naibu Waziri na kuongeza,
"Sisi ambao tuna husika na wananchi moja kwa moja kama wabunge, madiwani na wenyeviti ni mashahidi kwamba wananchi wetu bado wana ukosefu wa haki zao hasa masuala ya kisheria, kwa hiyo nina imani ninyi mkiwapa maarifa watu wanaokuja kusoma hapa mnakuwa mnasaidia kwenye eneo la haki."
Pia Naibu Waziri huyo wa Katiba na Sheria ameongeza kuwa amejifunza masuala mengi ya Chuo cha IJA na 
kuhusu changamoto za Chuo Cha IJA, amebainisha kuwa atakwenda kuzifanyia kazi pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria na viongozi wengine.
"Mhe. Waziri wa Katiba na Sheria alikuja hapa akapokea changamoto zenu, nami niwaambie tutakwenda kuzifanyia kazi na kazi yetu sisi ni kuwa kiungo ili kuona mnafanya kazi vizuri," amebainisha Mhe. Naibu Waziri.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha IJA ambae pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Paul F.Kihwelo amesema kuwa Chuo ni kitovu cha elimu na Utafiti kwa upande wa Mahakama na kwamba kimeendelea kuzalisha watu muhimu kwenye eneo la usimamizi wa haki.
Awali katika ziara hiyo, Mhe. Naibu Waziri huyo wa Katiba na Sheria alitembelea maeneo kadhaa ya Chuo, ikiwemo Maktaba, Hosteli ya Wanaume ya Benjamini Mkapa pamoja na viwanja vya michezo vya Chuo.
Katika hatua nyingine, Uongozi wa Chuo umempatia Mhe. Naibu Waziri zawadi za vitu mbalimbali yakiwemo machapisho ya Chuo.







 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Pauline Gekul akisaini Kitabu cha wageni Ofisini kwa Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) alipofanya ziara Chuoni IJA.



Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul(katikati) akizungumza jambo wakati akiwa katika Maktaba  ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA)..

Kulia ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) ambae pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt Paul F. Kihwelo na kulia ni Mkutubi wa Chuo cha IJA, Bw, Jackson Chacha.



Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul (kushoto) akiwa na   Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) ambae pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt Paul F. Kihwelo(kulia) mara baada ya kukagua Hosteli ya wanaume ya Benjamin Mkapa alipofanya ziara hapa Chuoni IJA.



Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) ambae pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt Paul F. Kihwelo(kulia) akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Pauline Gekul(hayupo pichani) aliyetembelea Chuo cha IJA hivi karibuni.


Wajumbe wa Halmashauri Tendaji ya Chama cha wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, habari na utafiti(RAAWU) Tawi la Lushoto wakimsikiliza Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul  alipofanya ziara Chuoni IJA.



Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) ambae pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt Paul F. Kihwelo(kushoto) akimkabidhi machapisho ya Chuo Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul alipofanya ziara hapa Chuoni IJA.


Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul akizungumza na Wajumbe wa Menejimeti ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto(IJA) na Halmashauri Tendaji ya Chama cha wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, habari na utafiti(RAAWU) Tawi la Lushoto na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, alipofanya ziara hivi karibuni hapa Chuoni IJA.