Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Thursday, February 16, 2023

IJA YAENDESHA MAFUNZO YA WASHAURI WALEZI KWA MAJAJI 12 WA MAHAKAMA KUU

Na Innocent Kansha - Mahakama

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mhe. Dkt. Paul Kihwelo jana tarehe 30 Januari, 2023 alifungua mafunzo kwa Majaji 12 wa Mahakama Kuu ya Tanzania waliteuliwa kushiriki kwenye programu ya majaribio ya namna bora ya kujengeana uwezo wa kiushauri kwa Majaji na Mahakimu hasa wakati wa kuamua mashauri bila kuingilia uhuru wa Mahakama “Pilot Mentorship Programme”.

Akizungumza katika hafla fupi ya ufunguzi wa mafunzo hayo uliyofanyika katika ukumbi wa mikutano ulipo jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki jijini Dodoma, Mhe. Dkt. Kihwelo alisema mafunzo hayo yanatokana na matunda ya ushirikiano baina ya Mahakama ya Tanzania na Mahakama ya Mzunguko ya Uingereza na Wales kubuni mpango wa majaribio wa namna ya kujengeana uwezo kishauri ili kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi wakati wa kutoa maamuzi ya mashauri kwa Maafisa wa Mahakama.

“Kupitia mafunzo haya ya na namna bora ya kujengeana uwezo wa kiushauri kwa Majaji na Mahakimu tutakubaliana namna ya uandaaji kitabu cha Mwongozo utakao tumika katika shughuli za namna ya kuanzisha mahusiano kushauriana kwa njia rasmi na zisizo rasmi ‘Mentor & Mentee Relationship’ wakati wa kuamua mashauri na migogoro inapowasilishwa Mahakamani” alisema Jaji Kihwelo

Mhe. Dkt. Kihwelo alisema program hiyo itategemea zaidi ushirikishwaji wa uzoefu na weledi mkubwa walionao Majaji hao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku hasa katika eneo la kutatua migogoro ama mashauri yanayolenga kupambana na rushwa kubwa zenye thamani ya kuanzia milioni 200 na kuendelea kwa ustawi wa Taifa.

“Program hii msingi wake utazingatia uhuru wa Mahakama kwa asilimia mia moja katika kufanya maamuzi ‘Mentorship programme’ haitamaanisha mshauriwa anapaswa kufuata yale yote aliyoelekezwa na mshauri katika kufikia maamuzi kama msingi wa maamuzi yake juu ya jambo fulani lililopo mbele yake. Programu hii inalenga kuwajengea uwezo Majaji na Mahakimu wa namna bora ya kuongeza ufanisi na weledi kupitia uzoefu walionao wakati wa kutoa maamuzi ya kimahakama”, alisisitiza Jaji Dkt. Kihwelo.

Mhe. Dkt. Kihwelo alisema kupitia Programu hiyo itakuwa ya msaada mkubwa kwa Mahakama ya Tanzania na kutoa matokeo chanya kwa maendeleo ya kazi kwa maafisa wa Mahakama. Kupitia forumu hiyo akawashauri Majaji  kuchangia mawazo yao kwa kutumia uzoefu mkubwa walionao ili kufanikisha mwongozo bora wa programu ya ushauri.

Mafunzo kama hayo shabaha yake kubwa ni kutoa msaada, kwatia moyo na kuwapatia mwongozo Maafisa wa Mahakama wale ambao hawakupata bahati ya kushiriki moja kwa moja programu ya mafunzo ya ‘Mentorship programme’. Majaji waliohudhuria mafunzo watatumika kutoa elimu hiyo na kuwajengea uwezo Maafisa wengine katika maeneo yao ya kiutawala

Programu itaangazia maeneo ambayo yanaathirika na kugubikwa kwa kiwango kikubwa na vitendo vya makosa ya rushwa na uhujumu uchumi kama vile Dar es salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha na Mbeya. Takwimu za mwezi mei, 2022 zinaonyesha kuwa mashauri 147 ya makosa hayo yanayoendelea katika Mahakama za Hakimu Mkazi katika miji tajwa, makosa 21 ni ya mtandao mkubwa wa makosa ya rushwa na yamebainishwa na mtandao wa Programu Endelevu wa Mapambano ya kuzuia Vitendo vya Rushwa Tanzania (BSAAT).

Jaji Dkt. Kihwelo alihitimisha kwa kuwashukuru wabia waliowezesha kufanikishwa kwa programu hiyo ambao ni Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania na Ofisi ya Maendeleo ya Jumuiya ya Madola, kupitia Programu yake endelevu ya kupambana na Vitendo vya Rushwa Tanzania “The British High Commission (Foreign, Commonwealth & Development Office – FCDO through the Building Sustainable Anti – Corruption Action in Tanzania (BSAAT)”.