Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Thursday, December 14, 2023

SERIKALI YA WANACHUO YAPATA MAFUNZO ELEKEZI

 Na Rosena Suka, IJA

Kaimu Mkuu wa Chuo na Naibu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Taaluma, Tafiti na Ushauri, Bw. Goodluck Chuwa leo tarehe 14 Desemba, 2023 amefungua mafunzo elekezi ya siku moja kwa Viongozi wa Serikali ya Wanachuo wa IJA (IJASO) kwa mwaka wa masomo 2023/2024 yaliyofanyika Chuoni Lushoto.

Kwenye ufunguzi huo  Bwana Chuwa amewaeleza viongozi hao  kwamba lengo kuu la mafunzo hayo elekezi ni kuwajengea uwezo kwenye utekelezaji wa  majukumu yao ya uongozi kwa kufuata miongozo ya sheria, taratibu na kanuni za chuo na taifa kwa ujumla. 

Bwana Chuwa aliendelea kwa kusema viongozi hao wamebeba dhamana kubwa ya kuwahudumia wanachuo wenzao  kwa sababu wao ni kiungo  katika kuwafikisha maelekezo yote yanayotolewa na Menejimenti kwenda kwa wanachuo na kutoa mrejesho kutoka kwa wanaowangoza kuja kwenye menejimenti bila kuongeza au kupunguza uhalisia.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Fatihiya Massawe aliwasisitiza viongozi hao wa wanachuo kutendea haki nyadhifa walizonazo kwa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili waliowachugua kwani serikali ya wanachuo ni chombo muhimu katika musitakabali wa Chuo.

Prof. Masawe aliwakumbusha viongozi hao kusimamia sheria, kanuni na taratibu zilizopo ili kuonyesha mfano bora kwa wanachuo wenzao.

Katika semina hiyo elekezi viongozi hawa wamepitishwa katika mada mbalimbali zilizotolewa na watoa mada kutoka katika taasisi za umma Wilayani Lushoto ambao ni Mwakilishi kutoka Taasisi ya Kupambana na Rushwa (PCCB), Mwakilishi kutoka Jeshi la Polisi na Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).  Mada nyingine zilitolewa na vitengo na Idara vya ndani ya Chuo ambavyo ni Mkaguzi wa ndani, Mhasibu Mkuu,Mdhibiti ubora, Msajili na Mshauri wa Wanachuo.

Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kina utaratibu wa kutoa mafunzo elekezi kwa Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kila mwaka mara tu serikali hiyo inapowekwa madarakani.


Kaimu Mkuu wa Chuo na Naibu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Taaluma, Tafiti na Ushauri, Bw. Goodluck Chuwa akifungua Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO


Naibu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Fatihiya Massawe akiwaelekeza Viongozi wa Serikali ya Wanachuo katika  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO


Inspecta wa Polisi kutoka Wilaya Lushoto Karim Bruno akiwasilisha mada kwa Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO

Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Vya Taifa Wilayani Lushoto (NIDA) Bwana Francis Daniel akiwasilisha mada kwa Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO


Mwakilishi kutoka Taasisi ya Kupambana na Rushwa  Wilayani Lushoto (PCCB) Bwana Norbert Massaba akiwasilisha mada kwa Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO


Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO wakifuatilia mada

Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO wakifuatilia mada

Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO wakifuatilia mada

Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO wakifuatilia mada


Viongozi wa Serikali ya Wanachuo kwenye  Mafunzo Elekezi kwa Serikali ya Wanachuo  IJASO wakifuatilia mada