Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Saturday, January 27, 2024

SPKA WA BUNGE AZINDUA WIKI YA SHERIA

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson amezindua maadhimisho ya wiki ya sheria leo tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.

Katika uzinduzi huo Mhe. Dkt. Tulia  alikuwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo na amewataka washiriki wa maonesho hayo kuelimisha wananchi kwenye mambo mbalimbali yahusuyo sheria.

Sambamba na uzinduzi wa wiki ya sheria, Mhe. Dkt. Tulia pia amezindua rasmi Mfumo wa Udukuzi na Tafsiri (TTS) wa Mahakama ya Tanzania ambao utatumika katika kutafsiri na kunukuu lugha zinazotumika mahakamani mbazo ni Kiswahili na Kingereza na utakaorahisisha zaidi huduma ya upatikanaji haki kwa wananchi.

 “Naipongeza Mahakama ya Tanzania kwa hatua kubwa ya kuleta Mfumo huu, ambao naamini utarahisisha upatikanaji wa haki kwa wananchi,” amesema Mhe. Dkt. Tulia. 

 Aidha, Mhe. Dkt. Tulia ametoa rai kwa wadau wote wa Mahakama kufanya uwekezaji wa miundo mbinu ya TEHAMA ili kuendana na kasi ya Mahakama katika kuboresha utendaji kazi na kuongeza ubora wa huduma.

 ‘‘Naamini kazi kubwa sasa, hasa wadau wa Mahakama ni utengenezaji wa mfumo hasa wa kitehama, utakaowasaidia wadau hawa kufungamanisha na kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai unaosomana, ili kubadilishana taarifa kuanzia hatua ya upelelezi, ufunguaji wa mashauri, msaada wa kisheria, uendeshaji wa mashtaka, kusikiliza mashauri na utoaji uamuzi,” amesema Mhe. Dkt. Tulia. 

 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, akiwa anamkaribisha mgeni rasmi amesema, Mahakama ya Tanzania imewekeza kwenye matumizi ya TEHAMA kwa kuweka  Mifumo mbalimbali ili kurahisisha  huduma za utoaji haki kwa wananchi.

Mhe. Prof. Juma aliendelea kwa kueleza faida za mfumo huo  kuwa  utawaapunguzia  kazi Majaji na Mahakimu waliyokuwa wanaifanya ya kuandika kwa mkono mienendo ya mashauri kwa mfumo huu utarahisha na kufanya wananchi kupata haki kwa wakati.

Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto ni miongoni mwa Wadau mbalimbali wa Mahakama, ambapo wanashiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yaliyoanza tarehe 24 Januari mpaka 30 Januari, 2024. Wadau wengine wa Mahakama wanaoshiriki katika maonesho hayo ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Tume ya Haki za Binadamu, Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake (TAWJA), Polisi, Magereza na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).

Katika maadhimisho haya ya Wiki ya Sheria na Siku ya Sheria, kauli mbiu ni  “Umuhimu wa Dhana ya Haki kwa Ustawi wa Taifa: Nafasi ya Mahakama na Wadau katika Kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai.

Maonesho haya yaliyozinduliwa leo yatafanyika kwa muda wa siku nane ambapo yanatarajiwa kukamilika tarehe 30 Januari, 2024 ambapo yatahitimishwa kwa kilele cha Siku ya Sheria itakayofanyika tarehe 01 Februari, 2024 na mgeni rasmi wa siku hiyo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson akihutubia wananchi kwenye uzinduzi wa  maadhimisho ya wiki ya sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiwa na Viongozi wa Mahakama ya Tanzania kwenye matembezi kwa ajili ya uzinduzi wa  maadhimisho ya wiki ya sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.

Viongozi wakiwa katika matembezi maalum kwa ajili ya uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria yaliyofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.


Jaji wa Mahakama Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Chuo wakati wa  uzinduzi wa  maadhimisho ya wiki ya sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mhe. Dkt. Tulia Ackson(katikati) ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama ya Rufani.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mhe. Dkt. Tulia Ackson(katikati) ikiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa maonesho wiki ya sheria,

Baadi ya washiriki wa maonesho ya Wiki ya Sheria wakiwa wanafuatilia uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma


Aliyewahi kuwa mwanachuo IJA alipotembelea Banda la Chuo kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusiana na Chuo