Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Jaji kiongozi wa Tanzania

Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikakati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa stashahada ya sheria

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Mahafali ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto yaliyofanyia 18 Desemba, 2020

Saturday, February 24, 2024

UJUMBE WA BENKI YA DUNIA WATEMBELEA IJA

 Na: Rosena Suka, IJA

Leo tarehe 24 Februari, 2024 ujumbe wa Benki ya Dunia umetembelea mradi wa ujenzi wa studio ya jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’ unaofanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto.  Mradi huo ni kati ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mahakama ya Tanzania kwa ufadhili wa Benki wa Benki ya Dunia.

Ziara hiyo imewakilishwa na Maafisa wanne kutoka Benki ya Dunia ukiwa unaongozwa na Bi. Christine Owuor na Maafisa wengine watatu. Pamoja na Maafisa hao pia kulikuwa na watumishi kadhaa wa Mahakama ya Tanzania akiwemo  Jaji Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Maboresho, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Dkt. Angelo Rumisha.

Baada ya kuwasili Chuoni ujumbe huo ulifika katika eneo la Mradi wa ujenzi wa Studio jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’ ambao umeanza tarehe 18 Februari, 2024 na unategemea kumalizika tarehe 18 Mei. 

Ujumbe huo pia ulipata maelezo ya uundwaji na matumizi ya studio hiyo itakavyo fanya kazi kutoka kwa Mhandishi Emmanuel Mbosso wa Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo. Pia alieleza kwa ugeni kuwa Jukwaa la kujifunzia mtandaoni limetengenezwa na wataalamu wa ndani ya Tanzania ambao ni kutoka Mahakama ya Tanzania, Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Chuo cha Serikali za Mitaa (Hombolo).

Jukwaa la mafunzo ya mtandao litarahisisha utoaji wa mafunzo kwa watumishi  wengi wa mahakama, kwa  gharama nafuu na kupunguza umbali wa kufuata mafunzo. 


Picha ya pamoja ya Maafisa wa Benki ya Dunia waliotembelea mradi wa ujenzi wa studio ya jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’ unaofanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto. Waliokaa katika ni Bi. Christine Owuor ambaye Kiongozi wa Ujumbe kutoka Benki ya Dunia. Kushoto ni Jaji wa Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Mhe. Dkt. Paul Faustin Kihwelo na Kulia ni Jaji Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Maboresho, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Dkt. Angelo Rumisha. na waliosimama nyuma ni Maafisa wa Benki ya Dunia.

Picha ya juu na ya chini ni watumishi wa IJA na Mahakama waliokuwa kwenye mapokezi ya ugeni wa wakilishi wa Benki ya Dunia wakifuatilia taarifa mbalimbali zilizokuwa zinatolewa kuhusu mradi ujenzi wa  wa studio ya jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’ unaofanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto. 


Mhandishi Emmanuel Mbosso wa Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo akitoa maelezo ya uundwaji wa studio ya jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’



Picha ya juu na chini ni Wajumbe wa Benki ya Dunia na Viongozi wa Mahakama ya Tanzania  wakipata maelezo ya mradi wa ujenzi studio ya jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’ kutoka kwa Mhandisi wa mradi huo.


Meza kuu na viongozi kutoka Mahakama ya Tanzania


Meza Kuu na Sekretarieti

Meza kuu na Baadhi ya watumishi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto


Meza Kuu na baadhi wa watalaamu walioshiri kutengeneza jukwaa la kufundishia kwa njia ya mtandao ‘e-learning’ 
















Saturday, January 27, 2024

SPKA WA BUNGE AZINDUA WIKI YA SHERIA

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson amezindua maadhimisho ya wiki ya sheria leo tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.

Katika uzinduzi huo Mhe. Dkt. Tulia  alikuwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo na amewataka washiriki wa maonesho hayo kuelimisha wananchi kwenye mambo mbalimbali yahusuyo sheria.

Sambamba na uzinduzi wa wiki ya sheria, Mhe. Dkt. Tulia pia amezindua rasmi Mfumo wa Udukuzi na Tafsiri (TTS) wa Mahakama ya Tanzania ambao utatumika katika kutafsiri na kunukuu lugha zinazotumika mahakamani mbazo ni Kiswahili na Kingereza na utakaorahisisha zaidi huduma ya upatikanaji haki kwa wananchi.

 “Naipongeza Mahakama ya Tanzania kwa hatua kubwa ya kuleta Mfumo huu, ambao naamini utarahisisha upatikanaji wa haki kwa wananchi,” amesema Mhe. Dkt. Tulia. 

 Aidha, Mhe. Dkt. Tulia ametoa rai kwa wadau wote wa Mahakama kufanya uwekezaji wa miundo mbinu ya TEHAMA ili kuendana na kasi ya Mahakama katika kuboresha utendaji kazi na kuongeza ubora wa huduma.

 ‘‘Naamini kazi kubwa sasa, hasa wadau wa Mahakama ni utengenezaji wa mfumo hasa wa kitehama, utakaowasaidia wadau hawa kufungamanisha na kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai unaosomana, ili kubadilishana taarifa kuanzia hatua ya upelelezi, ufunguaji wa mashauri, msaada wa kisheria, uendeshaji wa mashtaka, kusikiliza mashauri na utoaji uamuzi,” amesema Mhe. Dkt. Tulia. 

 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, akiwa anamkaribisha mgeni rasmi amesema, Mahakama ya Tanzania imewekeza kwenye matumizi ya TEHAMA kwa kuweka  Mifumo mbalimbali ili kurahisisha  huduma za utoaji haki kwa wananchi.

Mhe. Prof. Juma aliendelea kwa kueleza faida za mfumo huo  kuwa  utawaapunguzia  kazi Majaji na Mahakimu waliyokuwa wanaifanya ya kuandika kwa mkono mienendo ya mashauri kwa mfumo huu utarahisha na kufanya wananchi kupata haki kwa wakati.

Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto ni miongoni mwa Wadau mbalimbali wa Mahakama, ambapo wanashiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yaliyoanza tarehe 24 Januari mpaka 30 Januari, 2024. Wadau wengine wa Mahakama wanaoshiriki katika maonesho hayo ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Tume ya Haki za Binadamu, Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake (TAWJA), Polisi, Magereza na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).

Katika maadhimisho haya ya Wiki ya Sheria na Siku ya Sheria, kauli mbiu ni  “Umuhimu wa Dhana ya Haki kwa Ustawi wa Taifa: Nafasi ya Mahakama na Wadau katika Kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai.

Maonesho haya yaliyozinduliwa leo yatafanyika kwa muda wa siku nane ambapo yanatarajiwa kukamilika tarehe 30 Januari, 2024 ambapo yatahitimishwa kwa kilele cha Siku ya Sheria itakayofanyika tarehe 01 Februari, 2024 na mgeni rasmi wa siku hiyo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson akihutubia wananchi kwenye uzinduzi wa  maadhimisho ya wiki ya sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiwa na Viongozi wa Mahakama ya Tanzania kwenye matembezi kwa ajili ya uzinduzi wa  maadhimisho ya wiki ya sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.

Viongozi wakiwa katika matembezi maalum kwa ajili ya uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria yaliyofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.


Jaji wa Mahakama Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Chuo wakati wa  uzinduzi wa  maadhimisho ya wiki ya sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma.


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mhe. Dkt. Tulia Ackson(katikati) ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama ya Rufani.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mhe. Dkt. Tulia Ackson(katikati) ikiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa maonesho wiki ya sheria,

Baadi ya washiriki wa maonesho ya Wiki ya Sheria wakiwa wanafuatilia uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Sheria uliofanyika tarehe 27 Januari, 2024 katika Viwanja vya Nyerere ‘Square’ jijini Dodoma


Aliyewahi kuwa mwanachuo IJA alipotembelea Banda la Chuo kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusiana na Chuo