Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Friday, June 24, 2022

IJA YASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO NA TAASISI YA PAMS FOUNDATION

Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kimeingia makubaliano ya Ushirikiano na Taasisi ya PAMS Foundation wenye lengo la kuwajengea uwezo maafisa wa Mahakama wa namna bora ya kuendesha mashauri yahusuyo makosa dhidi ya wanyamapori pamoja na makosa mengine ya uhalifu wa kimataifa (international serious crimes).

Makubaliano hayo yanalenga pia kuijengea uwezo IJA katika eneo la utafiti kwenye maeneo ya makosa makubwa ya kimataifa ikiwemo makosa ya ujangili wa wanyama pori na misitu.

Makubaliano hayo yamesainiwa leo tarehe 23/06/2022 jijini Dar es Salaam kati ya Jaji Dkt. Paul Faustin Kihwelo, Jaji wa Rufani na Mkuu wa Chuo pamoja na Bi Krissie Clark, Mkurugenzi Mtendaji na miongoni mwa waasisi wa PAMS Foundation yenye Makao yake makuu jijini Arusha.

PAMS Foundation ni shirika lisilo la kiserikali  lenye dhamira ya kuwawezesha wale wote wanaolinda wanyamapori na misitu.




Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, ambaye pia ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya PAMS Foundation, Bi. Krissie   Clark (kushoto), wakibadilishana mkataba huo


Mkurugenzi wa Operationi na Mafunzo, Bw.Samson Kassala( wa kwanza kushoto)na na  Mkurugenzi wa Intelijensia na Uchambuzi,(wa pili kushoto) Bw.Elisifa  Ngowi wakisaini mkataba huo. 


Mkurugenzi wa Operationi na Mafunzo, Bw.Samson Kassala( wa kwanza kushoto)na na  Mkurugenzi wa Intelijensia na Uchambuzi,(wa pili kushoto) Bw.Elisifa  Ngowi wakifuatilia utiaji saini huo. 




Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, ambaye pia ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto , Mhe. Dkt. Paul Kihwelo (kulia) akimpatia machapisho mbalimbali ya Chuo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya PAMS Foundation, Bi. Krissie   Clark (kushoto).


0 comments:

Post a Comment