Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kimeingia makubaliano ya Ushirikiano na Taasisi ya PAMS Foundation wenye lengo la kuwajengea uwezo maafisa wa Mahakama wa namna bora ya kuendesha mashauri yahusuyo makosa dhidi ya wanyamapori pamoja na makosa mengine ya uhalifu wa kimataifa (international serious crimes).
Makubaliano hayo yanalenga pia kuijengea uwezo IJA katika eneo la utafiti kwenye maeneo ya makosa makubwa ya kimataifa ikiwemo makosa ya ujangili wa wanyama pori na misitu.
Makubaliano hayo yamesainiwa leo tarehe 23/06/2022 jijini Dar es Salaam kati ya Jaji Dkt. Paul Faustin Kihwelo, Jaji wa Rufani na Mkuu wa Chuo pamoja na Bi Krissie Clark, Mkurugenzi Mtendaji na miongoni mwa waasisi wa PAMS Foundation yenye Makao yake makuu jijini Arusha.
PAMS Foundation ni shirika lisilo la kiserikali lenye dhamira ya kuwawezesha wale wote wanaolinda wanyamapori na misitu.
Mkurugenzi
wa Operationi na Mafunzo, Bw.Samson Kassala( wa kwanza kushoto)na na
Mkurugenzi wa Intelijensia na Uchambuzi,(wa pili kushoto) Bw.Elisifa
Ngowi wakifuatilia utiaji saini huo.
Jaji
wa Mahakama ya Rufani Tanzania, ambaye pia ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama
Lushoto , Mhe. Dkt. Paul Kihwelo (kulia) akimpatia machapisho mbalimbali ya Chuo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya PAMS Foundation, Bi. Krissie
Clark (kushoto).











0 comments:
Post a Comment