Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Tuesday, November 8, 2022

IJA YATOA MAFUNZO YA UENDESHAJI WA MASHAURI YA MAKOSA YA KIFEDHA


Mhe. Amiri Mruma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam amefungua mafunzo ya uendeshaji wa mashauri Makosa ya Kifedha (Financial Crimes) kwa maafisa wa Mahakakama 30 katika ukumbi wa Lamada jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayo ya siku tano kuanzia leo tarehe 07/11/2022  yameandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Eastern and Southern Africa Anti-Money Laundering Group (ESAAMLG) na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).

Washiriki wa mafunzo hayo ni Majaji 14 pamoja na Mahakimu Wakazi 26 ambapo kati yao 24 ni Mahakimu Wakazi wa Mikoa Tanzania Bara. Lengo la mafunzo hayo ni kuwafanya washiriki hao waweze kubadilishana uzoefu kwenye maeneo mbalimbali ya sheria za kimataifa na kitaifa za biashara haramu ya wanyamapori, ufadhili wa ugaidi na utakatishaji fedha, kuangalia madhara ya makossa hayo katika taifa na dunia,   urejeshaji wa mali zilizopatikana kutokana na makosa hayo, wajibu wa Maafisa wa Mahakama, wapelelezi na waendesha mashtaka katika uendeshaji wa mashauri yahusuyo makosa hayo n.k.

Wawezeshaji wa mafunzo hayo ni baadhi ya majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, ofisi ya Mashtaka ya Taifa, Wizara ya Maliasili na Utalii, PPRA, wawezeshaji kutoka mamlaka za wanyamapori za baadhi ya nchi barani Afrika na wawezeshaji wabobevu kutoka mataifa mbalimbali duniani.

Mafunzo haya ni muendelezo wa mafunzo mengine kama hayo yaliyotolewa kwa kundi la kwanza la Mahakimu 40 mwezi Septemba mwaka  huu.

Pichani juu Mhe. Amiri Mruma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam (katikati) alipokuwa anafungua mafunzo ya mafunzo ya uendeshaji wa mashauri Makosa ya Kifedha (Financial Crimes) kwa maafisa wa Mahakama kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara ambao wanaonekana kwenye picha za chini.








0 comments:

Post a Comment