Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Tuesday, December 6, 2022

JUMUIYA YA WAHITIMU IJA YAENDESHA KONGAMANO LA KITAALUMA

 Na Rosena Suka, IJA

Mhe. Dkt. Gerald Ndika, Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo Desemba 6,  2022  amefungua Kongamano la Kitaaluma lililoandaliwa na Jumuiya ya Wahitimu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA ALUMNI) katika ukumbi wa Barnabas Samatta Chuoni Lushoto.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo Mhe. Dkt. Ndika alianza kwa kuwapongeza wanajumuiya hao kwa kujitolea na kushiriki katika shughuli mbalimbali zenye nia ya kutoa elimu na kukuza uelewa katika jamii kuhusiana na masuala ya sheria ikiwepo kuandaa makongomano ya kitaaluma kama hilo, kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi bure na kushiriki katika masuala mbalimbali yanayoandaliwa na Chuo kwa lengo la kuwaunganisha na kuwajengea umoja wahitimu wote wa chuo.  

Mhe. Dkt. Ndika aliendelea kwa kusema kongamano hilo ni fursa nzuri kwa washiriki kudadavua masuala muhimu yahusuyo mambo mbalimbali ya kiuchumi na ya kijamii, sambamba na kuangalia ukuaji katika maeneo ya utoaji haki.

 “ Na ni mategemeo ya Chuo na Taifa kwa ujumla kwamba kila mmoja wenu mara baada ya kuhitimu kwenu mnapaswa kuelewa kwamba nafasi nliyonayo ni vema mkaitumia katika kuleta maendeleo ya nchi na jamii kwa ujumla ili kukuza taaluma na kuielimisha jamii katika utoaji haki, mkizingatia usawa, Amani na usalama” alisema Mhe. Dkt. Ndika.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akiwa anafunga kongamano hilo aliwahimiza washiriki wa kongamano  kutumia fursa hiyo ili kuwa na mahusiano mazuri na kuitumia Jumuiya ya Wahitimu hao ili kupata fursa mbalimbali za kujifunza katika taaluma waliyonayo.

Kongamano hilo lililowashirikisha wanachuo wote lililoongozwa na mada isemayo “IJA and Prospects for offering practical legal training to lawyers Employed in Public Service ; Practicalities and Challenges” na hufanyika mara moja kila mwaka siku moja kabla ya sherehe za mahafali ya Chuo.

Mkuu wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo akiwa katika picha ya pamoja na Jumuiya ya Wahitimu wa IJA  baada kufungwa kwa kongamano hilo.




Picha mbalimbali za washiriki wakiwa wanafuatilia Kongamano











0 comments:

Post a Comment