Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Wednesday, May 25, 2022

JAJI MKUU WA UGANDA AFANYA ZIARA IJA

Jaji Mkuu wa Uganda, Mhe. Alfonse Chigamoy Owiny-Dollo leo tarehe 25 Mei, 2022 amefanya ziara ya kutembelea Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto na kujionea shughuli mbalimbali zinafanywa na Chuo.

 

Katika ziara yake, Mhe. Owiny-Dollo ameambatana na Maafisa 12 kutoka nchini Uganda ambao  miongoni mwa aliombatana nao ni Jaji Kiongozi wa Uganda Mhe. Dkt. Flavian Zeija, Msajili ya Mahakama ya Uganda, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa JTI Uganda, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya JTI Uganda, Msajili waTaasisi ya JTI Uganda na viongozi wa International Development Law Organization Uganda(IDLO).

 

Akiongea akiwa kwenye ziara hiyo, Mhe. Owiny-Dollo alisema kuwa  lengo la ziara yao ni kwa ajili ya kubadilishana uzoefu wa jinsi ya kuwandaa Maafisa Mahakama ambao wamepangiwa majukumu mapya na kujifunza jinsi ya kuijengea uwezo Taasisi ya Mafunzo ya Kimahakama ya nchini Uganda (JTI) pia  kujenga ushirikiano katika masuala mbalimbali yanayohusu vyuo na jinsi ya  kuiwezesha Mahakama ya Uganda kufanikisha katika maboresho yake kiutendaji.

Mhe. Owiny-Dollo aliendelea kwa kusema kuwa mafunzo ya kuwandaa Maafisa wa Mahakama wanaopewa majukumu mapya ni muhimu katika kuhakikisha kuwa kunakuwepo huduma bora ya utaoji haki kwa wananchi.

Alisema wanataka kupata uzoefu ambao utawasaidia yeye na ujumbe kutoka Chuo cha Mahakama cha Uganda kuwawezesha watumishi wanaopewa majukumu mapya kupata mafunzo ambayo yatasaidia katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

“Maafisa wa Mahakama walioandaliwa kwa kupewa mafunzo mazuri wataelewa vema majukumu yao na mambo ambayo anatakiwa kufanya katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma za kupata haki wanapokuwa na mashauri” alisema

Alipokuwa akiwakaribisha wageni hao, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Gerald Ndika alionyesha furaha yake kwa kuushuru ugeni huo kwa kusema kwamba ujio wao ni fursa muhimu ambapo wataitumia kwa kujifunza mambo mbalimbali na kubadilishana uzoefu jinsi vyuo vya Mahakama vinavyofanya kazi.

Naye Mkuu wa Chuo na  Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Dkt. Paul Kihwelo alipokuwa anaelezea historia ya Chuo kilianzishwa kwa Sheria ya Bunge, Sheria Namba 3 ya 1998. Kilianza kazi yake tarehe 23 Oktoba, 2000 na kilikuwa kinatoa Cheti na Diploma ya Kozi za Sheria. Uzinduzi rasmi ulifanywa na Rais Benjamin Mkapa tarehe 3 Agosti 2001.  Pamoja na historia hiyo Mkuu wa Chuo alieleza lengo la madhumuni ya kuanzishwa kwa Chuo ilikuwa ni kujengea uwezo watumishi wa Mahakama.

Ziara hiyo ni sehemu ya ushirikiano kati ya Mahakama ya Tanzania na Mahakama ya Uganda na ujirani mwema kati ya nchi hizi mbili. Sambamba na kutembelea maeneo mbalimbali ya Chuo, Wageni hawa wamepata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vilivyopo katika Wilaya ya Lushoto.


Jaji Mkuu wa Uganda, Mhe. Alfonse Chigamoy Owiny-Dollo alipokuwa anatoa 
salamu kwa viongozi wa IJA

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Gerald Ndika 
akitoa neno la ukaribisho kwa Jaji Mkuu wa Uganda na Viongozi wengine wa Mahakama ya Uganda.



Mkuu wa Chuo na  Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Dkt. Paul Kihwelo alipokuwa akiwaeleza wageni juu ya historia ya Chuo na shughuli Chuo kinazozifanya

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya JTI Uganda, Mhe. Damilie Lwanga akieleza kwa ufupi shughuli zinazoendeshwa na chuo hicho




Katika picha ni baadhi ya viongozi waliombatana katika Ziara ya Jaji Mkuu wa Uganda wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Uongozi wa IJA kuhusu utendaji kazi wa Chuo
Menejimenti ya IJA wakifuatialia maelezo yaliyokuwa yanawasilishwa na upande wa wageni kutoka Mahakama ya Uganda

Picha ya Mahakimu kutoka Wilaya ya Lushoto wakifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa inawasilishwa 
Picha ya pamoja ya Jaji Mkuu wa Uganda, Mhe. Alfonse Chigamoy Owinyi- Dollo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Uganda.


Picha ya pamoja ya Jaji Mkuu wa Uganda, Mhe. Alfonse Chigamoy Owinyi- Dollo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimienti ya IJA.

0 comments:

Post a Comment